HEADING ANIMATIONS

HEADING ANIMATIONS

FANYA KAZI YA MUNGU

FANYA KAZI YA MUNGU

Monday, July 23, 2012

FILAMU YA "DUNIA HAINA HURUMA" KUANZA SASA

JAMES TEMU (UNCLE JIMMY), BAHATI BUKUKU, RULEA SANGA (BLOGER), DAVID ROBERT NA WENGINE KUJA NA FILAMU KALI YA KUMTUKUZA MUNGU WETU "DUNIA HAINA HURUMA"

Mwandishi: Rulea Sanga

Umefika wakati Mungu amezungumza na hawa watumishi wa Mungu kwa kuwapa maono ya kutengeneza filamu ya "Dunia Haina Huruma". Ujumbe huu unatoka katika nyimbo mpya ya mwimbaji maarufu Tanzania, Bahati Bukuku inayoitwa "Dunia haina Huruma" Nyimbo hii imekuwa gumzo jijini Dar es Salaam kutokana na ujumbe wake unaogusa maisha ya watu na kukuweka karibu sana na Mungu unapousikia. Kama hujawahi kuusikia, nakuomba ujitahidi kusikiliza Praise Power Radio na Wapo Radio utabarikiwa.

Mhusikaka mkuu wa filamu hii, Bahati Bukuku

Kutoka na wimbo huu, watumishi wa Mungu wameamua kukaa chini na kuuzambaza ujumbe huu kwa njia ya filamu. Kwahiyo utafaidika kuusikia kwa njia ya uimbaji na pia kwa njia ya maigizo.

Katika filamu hii kutakuwa na watumishi wa Mungu kama James Temu a.k.a Uncle Jimmy (ambaye ni mwigizaji wa filamu Tanzania na ni mtangazaji wa Praise Power Radio Tanzania, mbali na hapo ni blogger) , Rulea Sanga (ambaye ni blogger na ni graphic designer, na mwezi April 2012 alibahatika kuitwa na Nabii TB Joshua kutokana na kazii yake nzuri ya blogu), David Robert (huyu ni muimbaji wa nyimbo za injili Tanzania na ni mjasiliamali mkubwa sana Tanzania), Bahati Bukuku (Huyu ndiye mhusika mkuu wa filamu hii, ni mwimbaji wa nyombo za injili Tanzania na amekuwa baraka kwa wale waliosikia nyimbo zake), Riyama Ally (huyu ni mwigizaji wa filamu Tanzania, amefanya kazi nyingi katika uigizaji)

Wimbo wa Bahati Bukuku wa Dunia haina huruma unagusa sana mioyo ya watu, hasa wale walioko katika ndoa na wale wanaotaka kuingia katika ufalme wa ndoa. Kutokana na wimbo huo, mtumishi wa Mungu Bahati Bukuku akaamua kuja na wazo la kutengeneza filamu ambayo itaonyesha kila kitu alichokiimba katika wimbo huo.

Mshiriki mwingine wa filamu ya "Dunia haina Huruma", Blogger wa RUMA AFRIKA, Rulea Sanga. Hapa akiwa katika gari la Wise Men wa Nabii TB Joshua katika Synagogue ya THE SCOAN. Kumbuka mwezi Aprili 2012 aliitwa na Nabii TB Joshua kutokana na kazi yake nzuri ya blogu yake ya www.rumaafrica.blogspot.com

Kwa sasa kila kitu kuhusina na filamu hii kimeandaliwa, ila kilichobaki ni kumtafuta dada mrembo na mwenye kuvutia, kwani kuna sehemu inahitajika kwaajili ya dada ambaye ni mrembo sana. Kama wewe unajiona ni mrembo na uunajiamini na unaweza kuigiza tunaomba uwasiliane kwa namba hii +255 713-763939.


Kumbukeni haya yote yanafanyika kwaajili ya kumtangaza Kristo na kuonyesha kuwa hata sisi tuliokoka tunaweza kufanya vitu vikali na vizuri. Umefika wakati wa kupenda vilivyo vya Mungu na ku-support kazi ya Mungu. Support yako itatuwezesha kufanya vitu vikali. Mungu anatumia watu kufanikisha kile anachotaka kifanyike, na leo wewe utakuwa ni mmoja wa wale Mungu anapenda ushiriki katika ku-support kazi hii isonge mbele. Kama unamchango wako wowote tutashukuru sana kusikia na kupokea kwako, mchango unaweza ukawa na mawazo, fedha au vitu. Kama wewe ni mmiliki wa vyombo vya shooting unaweza ukajitokeza tukafanya kazi ya Mungu.

Kwa mujibu wa Bahati Bukuku, amesema filamu hii itakuwa ya utofauti na filamu za watu wengine kwani watu watakao shiriki filamu hii watapimwa uwezo wao wakufanya kazi napia watasafiri baadhi ya mikoa kukamilisha kusudio la filamu hii.
Wadau wa blogu hii endeleni kuitembelea, ili mfahamu kitu kinachoendelea.

Riyama Ally ni mtumishi wa Mungu na anacheza filamu za Kitanzania (Bongo Movie). Naye atashiriki katika filamu hii.

David Robert, ni mwimbaji wa nyimbo za injili Tanzania na mjasiliamali. Atashiriki
Uncle Jimmy , ni mwigizaji katika Bongo Movie na amecheza na waigizaji wakubwa Tanzania akiwaomo Ray, JB,O na wengine wengi. Katika filamu hii utaona kazi yake ya uigizaji katika muonekano mwingine.


NIKUPE KIONJO CHA TAMTHILIA

Bahati Bukuku alipigiwa simu na mwanamke mmoja ambaye alijitambuliha kuwa yeye ni mke mwenzake, alimpa taarifa mbaya akimwambia "Nenda kachukue mzoga wako Muhimbili" . Bahati Bukuku akiwa katika kutafuta marafiki zake kuulizia taarifa hizi ili kujua zaidi, aliamua kufika mochwari Muhimbili, na alipofika Muhimbili alikutana na taarifa mbaya za kuumiza moyo wake kutoka kwa wale waliokuwa hapo Muhimbili.
Bahati Bukuku aliingia chumba cha maututi na kuona mpenzi wake amepoteza fahamu na hawezi kumtazama. Nilijisemesha kuwa "Dunia haina huruma, haina fadhili, nani mwenye huruma anifariji, moyo unavuja damu kwa matatizo ninayopata."
Bahati Bukuku akamua kuwapigia ndugu wa mume wake Mbeya ili awaeleze yaliyomsibu, lakini cha kushangaza ni kwamba wote walimsusia. Akajaribu kuchukua kitabu cha Bank ili kuangalia kama kuna pesa kidogo zimsaidie, lakina cha kusikitisha anaona ATM haizomi nikimaanisha hakuna pesa. Hakuchoka akaenda kwa daktari na kutaka kumuuzia gari aina ya Vogi, lakini daktari anakataa na kusema haya magari yanakula mafuta sana kwahiyo sitoweza kuwa nalo. Akiangalia marafiki zake wanazidi kularua moyo wake kwa maneno makali.
Bahati Bukuku kila akimwaangalia mume wake anazidi kuchanganyikiwa na hawezi kuongea naye. Mashemeji zake hawataki kusaidia na kila akiomba msaada kutoka kwao, nao wanamwambia "Shemeji sisi tunaenda kuangalia mpira Ulaya" akiwaambia mawifi zake nao wanamwambia, "Wifi hatuwezi kukusaidia, tunaenda kucheza segere".
Bahati Bukuku akaamua kwenda tena kwa daktari kuomba asaidiwe. Na chanzo cha matatizo kikaanza hapo. Bahati akibdi azae na huyu daktari ili apate msaada, maana amehangaika sana bila ya kupata msaada, na mgonjwa hali yake ni mbaya sana.

Mzigo ukazidi kwa Bahati Bukuku, hali ikazidi kuwa mbaya sana, maana amefanya kosa la kufanya tendo la ndoa na daktari na kuzaa mtoto, na bado ndugu hawampendi.
Baada ya kupata nafuu kwa mgonjwa na kurusiwa nyumbani na kuendelea na maisha yake ya kwaida, Bahati Bukuku akamwambia kuwa nimezaa na daktari. Na hii nililifanya kutokana na kushindwa kupata msaada kutoka kwa ndugu na marafiki, wote walinikimbia, kwahiyo nikaamua kufanya hivyo kwa daktari ili nipate pesa ya kukusaidia upate matibabu.

Mume na Bahati Bukuku aliposikia habari hizo kuwa mke wake ana mtoto na daktari akachukua mapnga na kutaka kumuua.

Mume na Bahati aliondoka na baadae Bahati Bukuku akaitwa kijijini kwa mume wake. Alipofika kijijini akawasalimia, nao hawakuta kumjibu wala kumsikia. Kikao kikakaa kutaka kumhukumu, na wakamwambia Bahati Bukuku, "Kama unataka kuishi katika familia hii, mtoto auawe". Akamtazama mume wake na yeye akamtazama kwa hasira. Bahati aakjiuliza, amkimbile nani kwani ndugu, marafiki na mume wake hawamtaki.
Ndugu wakmuweka mtoto kati ili wampige mapanga, akatokea baba mmoja na kuwauliza, ambaye hana dhambi na awe wa kwanza kupiga panga huyu mtoto. Mume na Bahati Bukuku baada ya kusikia hilo aliomba msamaha kwa mke wake na kusema kuanzia leo hii ya dunia yameisha nataka kutengeneza na Mungu.

Bahati amegundua ya kuwa Mungu anaweza kujibu maombi na kusamehe. Hii ni stori fupi ya tamdhilia ambayo itakujia kwako, kuna mengi ambayo utayaona katika filamu hiyo, Utaona mazingira yatakyotumika, wahusika wanatavyokuwa serious kukuletea huu ujumbe.

Lakini nataka kukuuliza wewe mdau wangu, unafikiri Rulea Sanga, David Robert, Uncle Jimmy, Bahati Bukuku n, Riyama Ally anaweza kufaa katika kitengo kipi?

Kwa haraka haraka kuna wahusika wafuatao:

1. Mke wa yule mume mgonjwa
2. Mume ambaye ni mgonjwa
3. Dada aliyempigia simu mke wa yule mume
4. Marafiki /mashoga wa mke wa mume
5.Daktari
6. Ndugu wa mume
7. Watu waliokataa kumsaidia Bukuku akiwa na shida.
8. Ndugu aliyepigiwa simu na Bahati Bukuku
9. Wacheza segere
9. Ndugu waliomua kwenda Ulaya kuangalia mpira
10. Mtoto wa daktari ambaye aliambiwa akatwe mapanga
11. Mtu aliyewambia wasimkate mapanga
TUNAOMBA MAONI YAKO.

FILAMU YA SIKU YA MWISHO-666 KUTOKA WIKI HII

Source: Ruma Africa & Papa Sam

(Kuhusiana na habari zingine kuhusiana na hii filamu tembelea www.rumaafrica.blogspot.com na www.samsasali.blogspot.com. Tutatakuwa tunakuletea kinachoendelea)

Ile Filamu ambayo inasubiriwa kwa hamu kubwa hususani Jamii Ya Kikristo Ya Siku za Mwisho inakamilika wiki hii na Kabla ya Kuingia Sokoni Mapema Mwezi Ujao.
Katika Filamu hiyo ya kibongo ambayo Papaa Ze Blogger amecheza kama Apostle P Nizo, ambaye ni Mtume na Nabii mwenye Kanisa lenye Ishara na Miujiza mingi na Baraka kadha wa Kadha pasipo waumini wa Kanisa hilo kutambua kuwa Apostle Nizo ana "Source Of Power" isiyotoka Juu.
Filamu hiyo yenye maudhui ya Kuwakumbusha Wakristo kuhusu Siku Za Mwisho na Kurudi Kwa Yesu Kristo imesheheni Vipaji Lukuki Vya Wakristo Katika kufikisha Ujumbe kwa Jamii.

Hapa ndipo Wanapokuwa kwenye Ibada Zao Wakisali ...Its a Nice Scene

Kushoto kabisa ni Papaa Ze Blogger akicheza Kama Apostle ndani ya Scene hiyo akiwa amevaa tofauti na wengine sababu na nafasi yake katika Impact katika Jamii

Hapa Apostle Nizo Akiwa anafatilia Ibada kwa Unakini Mkubwa ndani ya Chumba Cha Siri

Hapa Papaa Ze Blogger akiecheza Kama Apostle P, akidaka "power'
Apostle P Nizo akiwa na Kisu tayari kwa Ibada Ya Sadaka....Its very interesting Scene

Wakuu Katika Katika Kujipanga Kimkakati Mara baada ya Ibada ya Chumba Cha Siri

Kulia ni Papaa Ze Blogger ambaye amecheza kama Anointed Apostle, Katikati ni Pastor Alex, ambaye amecheza kama Mfanyabiashara mkubwa ambaye pia ni Mzee wa Kanisa Wa Apostle Nizo, na Kushoto Ni Mwanadada amecheza kama Mwanaharakati wa Haki za Wanawake na Mjasiriamali ambaye yuko connected na "chumba cha siri'

Laurence akiwa mwenzake ambaye wamecheza kama Askari wanaokagua magari kama yana sticker ya 666 maana hutaweza nunua mafuta wala kuendesha gari kama haijagongwa 666.

Hawa Watu Watatu wametisha Sana katika Scene hii ya "Chumba Cha Siri" Mpaka Pastor Kaduma Mtunzi wa Filamu hiyo, na Director Wa Filamu hiyo Mr. Mtitu Wakapiga picha na Jamaa

Scene hii Jamaa akiwa ameandaa Part nyumbani kwake ambapo amealika ndugu jamaa na marafiki,

Wageni Waalikwa Mabibi na Mabwana wakifurahia Chakula nyumbani kwa Mtumishi ambaye baadae atabaki sababu kumbe alidai amebarikiwa na mungu kupata hela kumbe Kapiga EPA.
Shemeji Yangu Edna Luvanda akiwa ndani ya Scene ya Siku za Mwisho, Kulia ni Dorcas Sakani ndani ya Filamu.

Full Kula
Hapa Madaktari wakijiandaa ndani ya chumba Cha Operation kwa ajili ya kumuhudumia mgonjwa

Hapa Wakiendelea na Operation

Kazi Ikaendelea
 
Daktari Bingwa akiwa Kazini kwenye Scene

Wakiwa Ndani ya Chumba Cha Operation Yesu anarudi na Daktari Bingwa anatwaliwa, sokomoko waliobaki ndani ya Chumba Wamuhudumie Mgonjwa ama Wamtafute Dr. Bingwa waliyetwaliwa.

Saturday, June 30, 2012

WE ARE BUILT WITH WORD-TB JOSHUA

Wise Man Harry gave an inspiring message to launch the service, titled, “Love Everyone, Trust Only God”.  He said that one of the great lessons life itself teaches us is that trust should not be readily given because we are in a danger zone where everyone lies to his neighbour. Great businesses do not just happen without trust; our greatest mistakes will happen because of quick trust. He said the same people who were praising Jesus were the ones who later crucified Him. Many times Jesus found Himself where people rejected Him because of His ideology.
He said we cannot succeed alone but we need good, inspired and informed people to succeed in life, which was why Jesus had 12 disciples. Those in whom we choose to trust should be led by God each day; when we trust them, we trust God.
TESTIMONIES

Healed Of Ovarian Cyst Through The Anointing Water
Mrs Ntisili Seng, a South African, was suffering from an ovarian cyst and had visited many gynaecologists for medical attention, who eventually recommended that she go for an operation. Her sister, in possession of the Anointing Water from The SCOAN rushed to her aid and  advised her to administer it in faith. To her surprise, the symptoms of the cyst disappeared and upon further medical examination, she was confirmed to be healed and without any trace of the ovarian cyst. Speaking to the congregation and viewers, she advised that people should not lose hope because God is always in control.

Healed Of Hypertension Through The Anointing Water
Mr Hassan Ola, from Warri, Delta State, had been suffering from hypertension for four years for which he could not get a solution. The heart disease had taken him to many places because it had deprived him of paying attention to his business, as he could not walk even for 30 minutes. He said he faced “troubles all over”.
He was lucky to obtain Anointing Water which God used to perform the divine miracle in his life. Today, he said, “I feel better. I can walk for more than one hour with no problem”. He said, “There is power in this water. You only need to believe.


Delivered From Fatal Accident Through The Anointing Water
Pastor Henry Neaba, based in Ebonyi State, Nigeria came to The SCOAN on January 2012 for “spiritual upliftment”. After receiving prayer from  Prophet T.B. Joshua, he returned home, believing that his case was settled. On March 12th, his boss had asked him to oversee a project at a site but felt strangely uneasy about the prospect. He decided to pray with Anointing Water in Jesus’ name to ward off the fear. He then boarded a okada (motorbike) to move to the site when, after five minutes, a car crashed into the bike. Pastor Henry flew off the motorbike, his head smashing into the windshield of the car. He went into a coma, his body slumped in a pool of blood. While in the coma, he saw himself on a spiritual journey which he could not understand but he kept shouting the name, Jesus. He saw a light and eventually saw T.B. Joshua who asked him to go back and pulled him to face where he was coming from.
Immediately he opened his eyes and slowly sat up to the amazement of the crowd of onlookers.  Unable to believe that he had survived such a traumatic accident, they rushed him to the hospital. When he was discharged, someone blessed him with a brand new car after hearing of surprising survival! He advised that people should believe in God as “any man who puts his trust in God will never be put in shame”.
Obtained Breakthrough Through Anointing Water
Mr Nyao Molongo Benjamin, a Cameroonian, had visited The SCOAN in November, 2012 and was privileged to receive the Anointing Water from T.B. Joshua. He had come to the church in order to battle his poverty and wretchedness. The problem was so severe that even the land that he owned, he was unable to build anything on it.
In a step of faith, he anointed the land and his little money he had for business with the Anointing Water. In the space of just over a year, his life had been transformed! He was able to build a good house, acquire three cars and his wife safely delivered two healthy twin boys.
He came to fight poverty and failure but God fought for him through the medium of the Anointing Water. Glory be to God!
Delivered From Satanic Powers And Cultism

A video was replayed in which Mr Jonathan was delivered by Wise Man Christopher the previous week. During the deliverance, the evil spirit manifested saying that he was the “King of Umuedu” who operated with 7 demons. After his deliverance, he confessed his experiences as an occultic man who had been used by satan to destroy countless lives. He had discovered at a young age that he was reincarnated as an old woman who had unusual evil powers and taught him many things in his dreams about the spiritual world.
Now free and ready to denounce the world of darkness, he had returned to church with his bag of seven charms which he used to summon the demons. One by one, he explained the name and function of each charm used for destruction. Telling how the demonic powers had taken hold of him, he explained how at the age of 12, he had killed and eaten a monitor lizard after which he became spiritually fortified. He would work without suspicion, using the faces of other people to attack his victims such that they would never suspect him. He explained that he would cause confusion within families by using the face of one of the family members to attack, implicating that person and bringing accusations of witchcraft. He also explained that he had the demonic power to manipulate people to do things against their will, such as stealing and stabbing people with a knife. All these powers came through the sacrifices he made to the seven demons, and each sacrifice involved some form of blood.
Mr Jonathan testified that immediately after his deliverance, he experienced rest and peace of mind for the first time in his entire life. He said he was now going to burn all of the demonic idols and give his life completely to Christ. He advised everyone to put their total trust in God, stressing that the spiritual world is real and not to be taken lightly.
PROPHET T.B. JOSHUA’S SERMON

Prophet T.B.Joshua’s sermon to the congregation was an powerful one, built on the theme of faith. He titled it, ‘We Are Built With The Word’. Quoting the words of Jesus in John 15:7, “If you abide in Me, and My words abide in you, you willask what you desire, and it shall be done for youhe said that Christ and the Word are one and that when the Word dwells in us, it produces prayer fruits.
Expanding on the theme, T.B. Joshua said, “God’s power working through His Word and Spirit brings about a new birth. Christ gives being (life) to His Word. We can have His Word by studying and learning it but when it comes to the ‘being’ – that is, the life in that Word – it is Christ Himself that gives it. You cannot build one up spiritually on philosophies or theories about the Word or history of the Word; it is not possible. We are made spiritual by living in the Word and by the Word living in us.
Addressing the issue of faith, the man of God said that we must realize that God is Spirit (John 4:24) and faith in Him is a spiritual issue to be discerned and operated spiritually. He added that faith cannot be imitated; it must arise in each person’s heart. Referring to Ephesians 3:17 he said that Christ, who is the Author and Finisher of your life, can only become your Heavenly Father, Deliverer, Saviour, Redeemer and Healer through faith.
Finally, he encouraged the congregation saying that God is building Himself into us, making Himself a part of us, as the Word dominates, rules and sanctifies our spiritual nature. If our spiritual nature is sanctified, you have an Intercessor; Someone is praying for you, reigning in power for you.
The faith of the congregation was lifted up after the inspiring message as people then saw a practical demonstration that every Word of God is Spirit and life. They saw the very life of God transforming people’s situations from sickness to good health in the prayer line, from problem to solution through words of prophecy and from bondage to freedom through deliverance.
The service came to an explosive end with a powerful time of prayer with the five wise men, declaring that anything that has a beginning must have an end. And truly people went home with the firm belief that the end had come to their affliction, hard time and sickness in Jesus’ name!

Saturday, June 16, 2012

FILAMU KUTOKA KWA DADA KEMY ZENYE MAFUNZO MAZURI KWA JAMII..NUNUA NAKALA YAKO SASA




 DADA KEMY, NAWASALIMU KATIKA JINA LA YESU.
Kemy ni mwigizaji wa filamu ambaye kwa sasa nimeokoka nafanya kazi ya Mungu kwa nguvu zangu zote. Nakuomba na wewe mdau wangu uingie katika kazi ya Mungu wakati huu ambao umepewa nafasi ya kutosha. Utafika wakati utashindwa hata kutamka neno na nafsi yako itahitaji kusema jambo lakini nguvu yako ikashindwa kukuwezesha kusema hilo ambalo unataka kusema. Tufanye kazi ya Mungu 
 
Mbali ya hayo yote, nakukaribisha katika blogu hii mpya (www.gilgalentertainment.blogspot.com) ambayo utakuwa unapata Neno la Mungu na kujua Kampuni yangu ya Gilgal inafanya nini kuchangia jamii katika kazi ya BWANA. Kuna mengi utayajua kuhusiana na Gilgal, mojawapo ni uuandaji wa filamu, kusaidia jamii hasa wasiojiweza,

Usiweke machungu ndani ya moyo wako, yanaweza kukusababishia ukawa mbali na Mungu na kukuletea magojwa. Mtafakari Mungu wakati wa shida zako. Mwambie Mungu asemi na wewe na uombe nguvu zake zikuujie wakati wa mapito makali
 Furaha hundoa stree na mikunjo ya sura yako ewe mpendwa
 Sikia maoni yangu..mtumikie Mungu angali u hai..siku ya kufumba macho hutapata nafasi tena ya kumtangaza Kristo
 Matembezi ni bora, hukusaidia kujua yale ambayo ulikuwa huyajui. Hapa nikiwa Arusha kikazi
 Nakupenda sana ewe mdau wangu...Nakuomba muda wote uwe ni mtu wa furaha na achana na chuki. Raha jipe mwenyewe

Wakati wa shida na majaribu makali, mtegemee Mungu na usiangalie wanadamu.


Wednesday, June 13, 2012

MPIGIE KURA CHRISTINA SHUSHO, IPIGIE KURA TANZANIA, IINUE AFRICA
VIVA SHUSHO....VIVA TANZANIA
Christina Shusho,akihojiana na mablogaz wa Kitanzania katika hotel ya The Atriums iliyoko Sinza Africa sana
Siku ya jana jioni mablogaz wanaomiliki blogu za Kikristo Tanzania, Rulea Sanga, Uncle Jimmy, Sam Sasali, K-Junior, Martin Macele walikuwa na mahojiano na Christina Shusho katika hotel ya The Atriums Sinza Africasana kuhusiana na shindano kubwa lililoko machochoni pa mtumishi wa Mungu Christina Shusho.

Christina Shusho alimshukuru Mungu kwa kuweza kumtumia kama chombo kufikisha ujumbe kwa jamii kwa njia ya uimbaji na pia kuweza kushiriki katika Gospel Music Awards Africa. Pia aliwashukuru mablogaz kwa kazi yao nzito wanayofanya kumtangaza katika blogs zao na kupoteza muda wao kwaajili ya kumuinua Kristo.
Aliwaomba Watanzania na Africa nzima kumchangua Christina Shusho ili kuliwakilisha Bara la Africa,Tanzania na kumuweka Kristo juu ya vyote.
Christina Shusho ni mwimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania na amekuwa chachu kwa waimbaji wenzake na kwa watanzania kwa uimbaji wake na ujumbe naoutoa ambao umekuwa na mguso katika kukarabati imani za watu.
Christina Shusho anategemea ku-perform DAR LIVE siku ya jumapili, kwahiyo amewaomba Watanzania wote kufika mahali pale na kuweza kumpigia kura, kutakuwepo na mablogaz na kompyuta zao ambapo utakutana nao na watakuelekeza jinsi ya kupiga kura....

Tukutane Jumapili Dar Live
1.Emmy Kosgei-Kenya
2.Dena Mwana – Congo
3.Ntokozo Mbambo- South Africa
4.Rebecca- UK
5.Gifty Osei- Ghana
6.Kefee -Nigeria
7.Onos Ariyo- Nigeria
8.Diana Hamilton-UK
9.Christina Shusho -Tanzania
10.Lara George- Nigeria
VIVA SHUSHO, VIVA TANZANIA-MSIKILZE SHUSHO ALIPOKUWA ANAONGEA NA MABLOGAZ JANA THE ATRIUMS HOTEL SINZA AFRIKASANA
USIKOSE MTUMISHI WA MUNGU...NJOO TUFANYE KAZI YA BWANA KWA KUM-SUPPORT MTANZANIA MWENZETU 

KAMA ULIKUWA HUJUI KUHUSIANA NA MASHINDANO HAYA, TAFADHALI SOMA HAPO CHINI



Siku 18 zimebakia kabla ya pazia la upigaji kura kufungwa kwa waimbaji wa gospel barani Afrika, ambao wanawania tuzo mbalimbali kupitia Africa gospel music awards ambazo zinatarajiwa kutolewa siku ya jumamosi ya tarehe 7 mwezi wa 7 mwaka huu huko jijini London nchini Uingereza. Ambapo kama ilivyokuwa kwa mwaka jana mwimbaji wetu mmoja tu, ametutoa kimasomaso kwa kupendekezwa katika kuwania kupata tuzo hizo mwimbaji huyo si mwingine bali ni Christina Shusho, ambaye mwaka jana alitoka mikono mitupu lakini mwaka huu tukiungana kwa pamoja watanzania wote kwa kumpigia kura lazima atarudi na tuzo zote mbili alizopendekezwa kuwania.

Shusho yumo kwenye kuwania mwimbaji bora wa kike wa mwaka pamoja na mwimbaji bora wa mwaka Afrika ya mashariki, tuzo ambazo anawania na waimbaji wengine wanaofanya vyema kwenye gospel barani Afrika wakiwemo wakina Ntokozo Mbambo wa Afrika ya kusini na waimbaji wengine. Kikubwa ninachoweza kukwambia tukifanikiwa kuunganisha nguvu zetu kwa pamoja kwa kumpigia kura atakuwa nanafasi kubwa ya kutwaa tuzo hizo, kwasababu waimbaji wengine wanaowania tuzo hizo wengi wao wanatoka nchi moja hali ambayo itafanya kura zao kugawana kitu ambacho kitatupa nguvu ya kumwezesha Shusho kurudi na tuzo kwani Tanzania nzima kura zetu tunaelekeza kwake.

Mikakati mbalimbali inafanywa ili kuhakikisha kila mtu anashiriki katika upigaji kura kwakuwa hauhitaji kulipa ili kupiga kura, kikubwa unatakiwa ujiandikishe kwenye tovuti ya shindano hilo ambayo maelekezo yake yapo chini ya habari hii, zaidi kama nilivyoandika mikakati inafanywa ili kuhakikisha watanzania wanashiriki kikamilifu katika zoezi hili katika siku 18 zilizobaki. Hapo jana bloggers walikutana na Christina Shusho katika hoteli ya Atriums iliyopo Sinza jijini Dar es salaam ili kupanga mikakati zaidi ya kuweza kupata tuzo hizo ambazo faida yake ni kumwinua Yesu pamoja na kuitangaza nchi yetu ya Tanzania duniani. Natumai umenielewa ili kupiga kura ingia kwenye link hii na kufuata maelekezo chini yake.
http://www.africagospelawards.com/nominate.html


AGMA 2012 VOTING GUIDELINES
1. Click on the 'VOTE NOW' button.
2. Register your email address, confirm and submit.
3. Check your email (inbox) and you will find the link to vote.
4. If you do not find the link in your email inbox, please check your junk mail folder.
5. Once you have connected to the voting page please make your selections and submit (you can only vote for one nominee from each category).
6. You do not have to vote in every category.


ANGALIA BAADHI YA PICHA ZA BLOGGERS NA CHRISTINA SHUSHO HAPO JANA 
Kikao kikiendelea

Blogger Victor kulia akinukuu jambo kutoka kwa Christina Shusho
Rulea Sanga alipoamua kupiga picha ya pamoja
Shusho akieleza jambo kwa mabloggers
 Victor akizidi kuchangia nawazo yake
K-Junior akiwa busy na kuchukua maphotoz

Watumishi wa Mungu wakihakikisha kila kitu kinaenda sawa


Papaa akimuelezea Shusho mikakati ya mabloggerz kuhusiana na upigaji kura


Kutoka kulia ni Shusho, Martin Malecela pamoja na Victor Mboya wakimsikiliza Rulea Sanga akimpongeza Shusho kwa juhudi zake


Rulea Sanga akisikiliza kwa makini mchakato wa kupata tuzo ulivyo.


Mablogaz  na mchungaji aliyoko upande wa kulia


K-junior wa kwanza upande wa kulia akimsikiliza mchungaji wa Vijana


Hakika kikao kilinoga wajameni.

Unclejimmy


Kikako kikiendelea na mabloggerz Tanzania waliojikita kumtangaza Kristo

''Inuka maana shughuli hii yakuhusu wewe, uwe na moyo mkuu, ukaitende (Ezra 10;4)''.
VIVA SHUSHO, VIVA TANZANIA.